Friday, December 27, 2013

Wimbo kutoka Mpanda Katavi

I like 4shared file "Lwinga Dume Ft. Ran P - Tazama.mp3" - http://www.4shared.com/mp3/45dA2woU/Lwinga_Dume_Ft_Ran_P_-_Tazama.html


Posted via Blogaway

Sunday, December 8, 2013

DR. SLAA APOPOLEWA MAWE KASURU KIGOMA

Katika hali ya kushangaza wanaojiita wafuasi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wamemrushia Mawe Katibu Mkuu wa Chama hicho wakati akihutubia mkutano wa chama mjini Kasuru.
Vijana hao wapatao kumi na tano waliokuwa na mabango yenye mbalimbali kama vile "Zit to kwanza Chadema baadae" walianza kumrushia mawe hali iliyopelekea askari Polisi kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) kumnusuru na kumficha sehemu ambayo mpaka tunakwenda mitamboni haikujulikana alipo.
Aidha polisi walitumia mabomu ya machozi kuwatawanya wafanya furugu hao hali iliyopelekea mkutano kuvunjika.
Katavi Up To Date inaendelea KufAnya utafiti wa chanzo cha vurugu hizo na wahusika wake...itaendelea kuwajuza kadri taarifa zitakavyokuwa zinapatika.


Posted via Blogaway

Tuesday, December 3, 2013

BACK ON AIR

Baada ya kimya kingi cha takribani miezi minne...blog yetu tuipendayo ya Katavi up to date inakuja tena kwa lengo lilelile la kukuhabarisha masuapa mbalimbali kuhusu mkoa wa katavi na duniani kwa ujumla....naamini msomaji utaifurahia blog hii na kuiona ya manufaa.....Aidha,  katika kuboresha upashanaji na upatikanaj habar basi mtu yeyote anayeweza kushiriki kutupia habari humu anakaribishwa...nitumie email adress yako katika nyambalatheman@gmail.com au katika nyambalamartin@yahoo.com...NYOTE MNAKARIBISHWA NA KATAVI NA TANZANIA NI YETU SOTE.


Posted via Blogaway

Sunday, June 9, 2013

TUPIA SWALI LOLOTE KUHUSU MUZIKI WA KIAFRIKA HAPA

Kwa habari za MUZIKI wa ki-AFRICA,Wanamuziki,Bendi zao,Historia zao na Maisha Yao kwa ujumla tembelea blog yetu...Acha swali linaLOmhusu Mwanamuziki Yeyote hapa Tanzania,DRC - Congo,Congo Republic na kwingineko Duniani.....!!!!!!!!!!!!!

Sunday, April 14, 2013

Aliyenyonga wanawe 2, kuua mke kizimbani


MKAZI wa kijiji cha Majimoto wilayani Mlele katika mkoa wa Katavi, Justine Albert (24) amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Mpanda akikabiliwa na makosa matatu ya mauaji.
 
Albert, juzi alifikishwa mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Kiganga Tegwa akishitakiwa kuwaua kwa kuwanyonga watoto wake wawili, Frank Justine (6) na Eliza Justine (4) huku miili yao akiitumbukizwa kisimani, kama mama yao aliyetumbukizwa akiwa hai lakini baadaye akafikwa na mauti.

Hata hivyo mshitakiwa huyo akiwa katika chumba cha mahakama kilichofurika watu hakutakiwa kujibu lolote, kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka kisheria kusikiliza shauri hilo ambalo litasikilizwa katika Mahakama Kuu.

Mwendesha Mashtaka, Mkaguzi wa Polisi, Ally Bwijo aliieleza mahakama hiyo kuwa mshitakiwa alitenda ukatili huo Aprili 6, mwaka huu saa 11:30 alfajiri ambapo aliwaua watoto wake hao wawili kisha miili yao na mama yao akiwa hai wakatumbukizwa katika kisima cha maji kijijini Majimoto.
Ilidaiwa pia kuwa mama huyo licha ya kuopolewa akiwa hai na kukimbizwa katika Kituo cha Afya kijiji Mamba, alifariki dunia Aprili 7, mwaka huu katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda alikohamishiwa kwa matibabu.

Monday, April 8, 2013

Madiwani Mpanda waandamana, wamkataa mkurugenzi mtendaji


MADIWANI wa Halmashauri ya Mji wa Mpanda mkoani Katavi wameandamana hadi ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo, Joseph Mchina wakitaka aondoke.

Madiwani hao wakiongozwa na Mbunge wa Mpanda Mjini, Said Arfi (Chadema) na Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo kabla ya kuanza maandamano hayo walikutana karibu na eneo la Shule ya Msingi Kashato.

Madiwani hao walipingana na umamuzi wa Mchina wa kuahirisha kikao cha Baraza la Madiwani kilichokuwa kifanyike jana, bila kutoa sababu za msingi.

Tuhuma alizotupiwa Mchina na madiwani hao ni pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo kutokuwa na ofisi hali inayomsababishia afanyie shughuli kwa kuomba chumba cha darasa shuleni.

Pia anadaiwa kuwa na tabia ya kuwagonganisha madiwani na watumishi na madiwani.

Tuhuma nyingine ni matumizi mabaya ya fedha na kukwepa kuitisha vikao vya sheria vikiwamo vya baraza la madiwani.

Akizungumzia msimamo huo wa madiwani, Arfi alidai kuwa kama Mchina yupo kwa maslahi ya watu fulani basi wamchukue wao na wakae naye ofisini kwao.

“Kama ni kisu sasa kimefika kwenye mnofu nikiwa na maana kuwa hatuko tayari kufanya tena kazi na Mchina (Mkurugenzi Mtendaji),” alisisitiza mbunge huyo.

UNYAMA KAMA HUU HAUVUMILIKI

  *Baba aua mke na watoto wawili kikatili.

  *Awanyonga na kuwatumbukiza kisimani

  *Kichanga anusurika, aokolewa akiwa hai

JESHI la Polisi mkoani Katavi, linamshikilia mkazi wa Kijiji cha Majimoto wilayani Mlele, Justine Albert (24), kwa kosa la kuwaua kikatili watoto wake wawili kwa kuwanyonga. na kisha kumjeruhi vibaya mke na kuwatumbukiza wote katika kisima kilicho karibu na kijiji hicho.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari alisema mauaji hayo yalitokea saa 11:30 alfajiri usiku wa kuamkia juzi.

Inasemekana kwa muda mrefu mtuhumiwa, alikuwa akimtuhumu mkewe kuwa na mahusiano ya kimapenzi na jirani yao na kwamba baadhi ya watoto wanadaiwa kuzaliwa nje ya ndoa yao.

Kwa mujibu wa chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya familia, watoto walionyongwa na baba yao ni Frank Justine (6),  na Elizabeth Justine (4), na mke wa mtuhumiwa, Jackline Lwiche (21) ambaye alifariki hospitali kwa matibabu.

Akisimulia tukio hilo ndugu wa Jackline anasema mama huyo ambaye alitumbukizwa kisimani akiwa hai alifanikiwa kumuokoa mtoto wake mmoja wa mwisho, Maria Justine mwenye umri wa miezi sita kwa kumtupa nje ya kisima, Maria Justine mwenye umri wa miezi sita.

Mama huyo aliyeopolewa majini na majirani akiwa hajitambui kwa kunywa maji mengi, na mtoto aliokotwa na majirani siku moja baada ya tukio akiwa na majeraha madogo mwilini mwake

Akisimulia mkasa huo, alisema kulipopambazuka baadhi ya wakazi wa kijiji hicho waliokuwa wakielekea kwenye shughuli zao, walimwona mtoto akiwa ametelekezwa kando ya njia na kumtambua kuwa ni Maria mwenye umri wa miezi sita, ambaye ni kitindamimba wa mtuhumiwa.
Inadaiwa ndipo walipoamua kufika nyumbani kwa mtuhumiwa na kumpatia taarifa hiyo na kuhoji alipo mama yake bila kupata majibu ya msingi.

Lakini mtuhumiwa aliwaeleza kuwa alikuwa ametoroka kusikofahamika na watoto wote.

Kutokana na maelezo hayo, wananchi hao walimtilia mashaka mtuhumiwa na kuamua kutoa taarifa kituo cha Polisi.

Baada ya polisi kwenda eneo la tukio, walimkuta kichanga (Maria) na kubaini ulikuwa na miburuzo ardhini na michubuko kitendo kilichowafanya wafuatilie mpaka kisimani.

Walipofika kisimani, waliamua kufungua mfuniko wa kisima hicho ndipo walikuta miili mitatu ikielea kwenye maji.

Kutokana na hali hiyo, polisi kwa kushirikiana na wananchi walifanikiwa kuopoa miili yote, huku mama ambaye alikuwa amekunywa maji mengi akiwa taabani na kupoteza fahamu.

Kamanda Kidavashari, alisema baada ya kumuopoa mama huyo alikimbizwa kituo cha afya cha kijijini Mamba, alilazwa hapo kwa matibabu hadi mauti yalipomfika jana  jioni. 

Saturday, April 6, 2013

BABU WA SAMUNGE AJA KIVINGINE

  • Adai kugundua unyayo wa mtu wa 182 baada ya Adam na Hawa
Mch. Ambilikile Mwasapile
MCHUNGAJI Ambilikile Mwasapile (78) ameibuka na kudai Mungu amemuonyesha unyayo wa mtu wa 182 tangu kuumbwa kwa Adamu. Masapila amekuwa maarufu kwa kutoa huduma ya dawa kwenye kikombe iliyodaiwa kutibu magonjwa sugu. Maelfu ya watu walikwenda kunywa “kikombe hicho cha Babu” mwaka juzi.

Akiwa ametanguliza sharti la kutopiga picha unyayo huo ulio kwenye jiwe alilolihifadhi nyumbani kwake, Masapila aliwaambia waandishi wa habari kuwa Mungu anaendelea kumuonyesha miujiza mingine.

“Nimepata unyayo wa mtu wa kale na Mungu ameniambia mtu huyo ni wa 182 tangu uumbaji wa Adamu na alikuwa binti anayeitwa Tutali.

“Tutali alikanyaga jiwe likazama kama mnavyoona huu ni unyayo wake… awali Mungu alinionyesha mahali ulipokuwa na akanielekeza nikaenda kuuchukua.

“Lakini mpaka sasa bado hajazungumza na mimi kwa ajili ya kuuweka hadharani hatua hiyo ni mpaka Mungu atakaponiruhusu,” alidai Masapila.

Alipoulizwa kama amewasiliana na wanasayansi waukague na kujiridhisha kama ni unyayo kweli, alisema hajafanya hivyo kwa vile anaendelea kumsikiliza Mungu.

“Hamfahamu bustani ya Eden ilikuwa kwenye hili eneo la Ngorongoro.

Niwaombe Watanzania waendelee kusubiri na wenye nia mbaya wataona maajabu zaidi,” alisema Masapila.

Akifafanua kuhusu huduma yake kupungukiwa na watu, Masapila alisema, mambo mengi yalichangia ikiwamo gharama za kufika nyumbani kwake kunywa dawa.

Thursday, March 28, 2013

MIAKA 30 JELA KWA UBAKAJI

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi ya Wilaya ya Mpanda, Mkoa wa Katavi, imemhukumu Pascal Fransisi (20) mkazi wa kijiji cha Igalula, kifungo cha miaka 30 jela, baada ya kupatikana na hatia ya kubaka mwanamke.

Hukumu hiyo, ilitolewa hapo jana na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda, Chiganga Tengwa, baada ya kuridhika na ushahidi wa mashitaka uliotolewa mahakamani hapo.

Awali mwendesha mashitaka, Ally Mbwijo, alidai mshitakiwa alitenda kosa hilo Februari 11, mwaka huu, saa 10 jioni nyumbani kwake.

Alidai siku hiyo, Fransins akiwa nyumbani kwake alimbaka mwanamke (jina tunalo) mkazi wa kijiji cha Kambanga, wakati akiwa anapita karibu na nyumbani kwake.

Alidai pamoja na mwanamke huyo kumkatalia kuingia ndani kwake, Fransis aliweza kufanikiwa kumwingiza ndani ya nyumba yake kwa nguvu.

Mshitakiwa baada ya kumwingiza ndani ya nyumba yake, alianza kumwingilia kwa nguvu kimwili, licha ya mwanamke huyo kupiga kelele za kuomba msaada.

Hakimu Chiganga, baada ya kusikiliza maelezo ya upande wa mashitaka na mshitakiwa aliridhika na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na ndipo alipomtaka mshitakiwa ajitetee kutokana na mahakama kumwona ana hatia.

Mshitakiwa Fransis katika utetezi wake, aliiomba mahakama isimpe adhabu kutokana na kile alichokieleza kuwa mwanamke huyo walikuwa na mahusiano naye ya kimapenzi.

Alidai mwanamke huyo aliamua kumshitaki baada ya kuwa wamemaliza tendo la ndoa na Fransis kushindwa kulipa fedha walizokubaliana.

Hakimu Chiganga, aliiambia mahakama kuwa mshitakiwa amevunja sheria ya kifungu namba 30 na 31 cha Kanuni ya Adhabu ya Marekebisho ya Sheria ya Mwaka 2002,

kwa hali hiyo mahakama imemtia hatiani, hivyo imemhukumu Fransis kwenda jela miaka 30 jela.

Wednesday, March 27, 2013

KATAVI NATIONAL PARK: How to reach and Enjoy the Park

Park regulations

Park rules and regulations

  • Plan your journey! Start your trip early because you must be back in the camp by 7 pm.
  • Unless you are specifically allowed to drive off-road, stay on the roads and tracks in all parts of the park. No game drives in the wilderness areas!
  • Be considerate to wildlife – do not harass, feed or interfere with wildlife. Do not get out of the vehicle when close to any animal!
  • Leave all plants, animals, skulls, bones, rocks or any other objects in the park where they belong.
  • Do not bring live animals or plants into the park.
  • Do not throw seeds of fruits and vegetables into the wild. They could start to grow.
  • Do not start fires unless at authorized camps.
  • Do not throw bottles, plastic bags, food waste from your car into the wild. Please make sure to take your trash with you or dispose it in proper dustbins.
  • Do not waste water.
  • Do not bring any firearms inside the park!
  • For your safety and safety of the wildlife, keep to the 50 km speed limit on all roads including the public roads Mpimbwe and Sumbawanga! Wildlife has the right-of-way everywhere in the National Park!
  • Do not cause any noise or create any disturbance which is likely to disturb other visitors and the animals.
  • Take precautions against malaria.
  • Tsetse biting has not yet caused medical problems in Katavi National Park.
  • Be aware of snakes!

Access

Best time to visit the park

Katavi National Park can be visited all year round. During the drier months (May to October and December to February), the animals congregate around the remaining water bodies and can be reached easily. During the wetter months, the extensive wetlands offer splendid scenery to adventurous visitors.

Location

Katavi National Park is located in Mpanda District, Rukwa Region in Western Tanzania. Currently, the main road that connects Mbeya and Sumbawanga with Mpanda town and Kigoma still crosses the park. The main entrance gate is close to Sitalike village, which is located along that main road 40 km south of the district capital Mpanda and 205 km north of the regional capital Sumbawanga.

Access to Katavi National Park

By air:
  • Fly directly to Katavi: This is the easiest way to reach Katavi at Sitalike or Ikuu airstrips. Another airstrip is available at Mlele
  • Safari Air Link runs the only scheduled flights between Katavi/Mahale to Ruaha, Selous, and Dar es Salaam/Zanzibar (Terminal 1 Julius Nyerere International Airport), P.O. Box 18065, Dar es Salaam, T: +255 777 (or 784) 723274, +255 783 397235, +441 452 862288, flights@flysal.com
  • Fly to Tabora or Kigoma: Regular flights are operated by Precision Air from Dar es Saalam to Tabora and Kigoma. From there you will have to continue by public transport or other arrangements.
By railway:
  • To Tabora and Mpanda: From Dar es Salaam regular trains go to Tabora from Tanzania Central Railways (from where they continue to Kigoma or Mwanza). From there a connection goes to Mpanda. The entire trip requires two travel days.
  • To Mbeya: By Tazara Railway or Bus from Dar es Salaam to Mbeya (Iyunga), then by road using public transport.
By road:
  • By road from Dar es Salaam/Mbeya: Drive to Mbeya in one day, then head to Sumbawanga and Sitalike/Katavi National Park. This is a two to three day safari (17hrs approximately).
  • Take the adventurous route and come by car from Arusha/Tabora: via Babati, Singida, Nzega and Tabora. There are two alternatives: Tabora to Mpanda or Tabora to Inyonga, Mlele and then to Sitalike/Katavi National Park.
  • By road from Kigoma via Uvinza and Mpanda to Katavi National Park.
From/to Mahale: Arrangements can be made from Katavi National Park HQ to go to Mahale National Park through Kabwe - Lukoma - Karema. If you are coming from Mahale National Park the arrangements can be made by the park warden.

Getting around inside the park

Hiring a vehicle is possible at TANAPA. A four-wheel drive car with a driver costs 100 US$ per day for 100 km
If you are driving yourself, you can obtain a map at the headquarters.
Hiring a guide (ranger) to the best places of Katavi is possible at the TANAPA headquarters.
Walking safaris guided by an armed ranger can be arranged.

Human Brain Analysis – Men vs. Women



1. MULTI-TASKING

Women – Multiple process
Womens brains designed to concentrate multiple task at a time.
Women can Watch a TV and Talk over phone and cook.
Men – Single Process
Mens brains designed to concentrate only one work at a time. Men can not watch TV and talk over the phone at the same time. they stop the TV while Talking. They can either watch TV or talk over the phone or cook.

2. LANGUAGE

Women can easily learn many languages. But can not find solutions to problems. Men can not easily learn languages, they can easily solve problems. That’s why in average a 3 years old girl has three times higher vocabulary than a 3 years old boy.

3. ANALYTICAL SKILLS

Mens brains has a lot of space for handling the analytical process. They can analyze and find the solution for a process and design a map of a building easily. But If a complex map is viewed by women, they can not understand it. Women can not understand the details of a map easily, For them it is just a dump of lines on a paper.

4. CAR DRIVING.

While driving a car, mans analytical spaces are used in his brain. He can drive a car fastly. If he sees an object at long distance, immediately his brain classifies the object (bus or van or car) direction and speed of the object and he drives accordingly. Where woman take a long time to recognize the object direction/ speed. Mans single process mind stops the audio in the car (if any), then concentrates only on driving.

5. LYING

When men lie to women face to face, they get caught easily. Womans super natural brain observes facial expression 70%, body language 20% and words coming from the mouth 10%. Mens brain does not have this. Women easily lie to men face to face.
So guys, do not lie face to face.

6. PROBLEMS SOLVING

If a man have a lot of problems, his brain clearly classifies the problems and puts them in individual rooms in the brain and then finds the solution one by one. You can see many guys looking at the sky for a long time. If a woman has a lot of problems, her brain can not classify the problems. she wants some one to hear that. After telling everything to a person she goes happily to bed. She does not worry about the problems being solved or not.

7. WHAT THEY WANT

Men want status, success, solutions, big process, etc… But Women want relationship, friends, family, etc…

8. UNHAPPINESS

If women are unhappy with their relations, they can not concentrate on their work. If men are unhappy with their work, they can not concentrate on the relations.

9. SPEECH

Women use indirect language in speech. But Men use direct language.

10. HANDLING EMOTION

Women talk a lot without thinking. Men act a lot without thinking.

Thursday, March 14, 2013

Mama auawa kwa kucharangwa Mapanga Itenka

MWANAMKE mmoja, Solile Juma (52) mkazi wa Kijiji cha Songambele, Kata ya Itenka, Wilaya ya Mlele mkoani Katavi ameuawa kwa kukatwakatwa mapanga wakati akiwa amelala nyumbani kwake. Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi, Joseph Myovela alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 9.00 usiku nyumbani kwa marehemu ambaye alikuwa akiishi na mwanae wa kike, Nkamba Chambani (15).

Alisema siku hiyo ya tukio Solile alikuwa na mwanae na baada ya kumaliza kula mlo wa usiku waliingia kulala, yeye akilala chumbani na mwanae sebuleni. “Ilipofika muda huo walisikia mlango ukivunjwa kwa kitu kizito na watu wasiofahamika idadi yao kisha kuingia ndani na kumtaka Solile atoe fedha zote alizokuwa nazo, lakini hakuwajibu,” alisema.

 Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda huyo baadaye walimshambulia kwa kumkatakata kwa mapanga sehemu mbalimbali za mwili huku mwanae ambaye walimkataza kupiga mayowe akishuhudia. “Baada ya kuona mama amefariki dunia watu hao walitokomea mahali kusikojulikana huku wakiwa hawajachukua kitu chochote,” alisema mtoto wa marehemu. Mtoto huyo alieleza kwamba baada ya kuona mama yake ameuawa aliendelea kukaa ndani hadi kulipopambazuka ndipo alipokwenda kumtaarifu babu yake, Juma Makoja ambaye naye alitoa taarifa kwa uongozi wa kijiji ambao nao walizitoa polisi.

Katika tukio hilo mtoto huyo hakujeruhiwa sehemu yoyote ile hali ambayo inaashiria kifo hicho kusababishwa na imani za kishirikina. Polisi wameahidi kuendelea na uchuguzi kuwasaka waliohusika na mauaji hayo.

 Source; Tanzania Daima

Wednesday, March 13, 2013

Mfahamu Papa Francisco wa I

George Mario Bergoglio-Papa Fransisco wa Kwanza
Jorge Mario Bergoglio,aliyezaliwa December 17, 1936 ndiye Papa mpya wa Kanisa Katoliki Duniani na Khalifa wa Mtakatifu Petro, amechaguliwa leo Tarehe 13.03.2013  na kuchukua jina la kichungaji la Papa Francico wa Kwanza, kabla ya kuchaguliwa kuwa Papa alikuwa Kardinali wa kanisa Katoliki nchini Argentina, alihudumu kama Askofu Mkuu wa Jimbo la Buenos Aires tangu mwaka 1998 na alipata cheo cha Kardinali mnamo mwaka 2001

Maisha yake

Jorge Bergoglio alizaliwa Buenos Aires, ni mmoja kati ya watoto watano watano wa  Baba wa kiItaliano aliyekuwa akifanya kazi katika Shirika la Reli nchini humo na mkewe. Baada ya kumaliza masomo yake ya Seminari huko Villa Devoto alijiunga na jumuiya ya Yesu Kristo mwezi Machi mwaka 11.03.1958 Bergoglio alijipatia shahada ya juu ya Filosofia katika chuo cha  Máximo San José huko San Miguel, na baadaye alifundisha Fasihi na saikolojia katika chuo cha Colegio de la Inmaculada huko Santa Fe, na chuo cha Colegio del Salvador huko Buenos Aires. alipata daraja takatifu la upadre  Desemba 13, 1969, aliopewa na Askofu Ramón José Castellano. alisomea masomo ya filosofia na Teolojia huko San Miguel.Bergoglio aliendelea huvyo na kuwa Professor wa Teolojia 

Papa Fransisco wa I akiwasalimia waamini wa Kanisa Katoliki na kutoa Baraka zake za kwanza kama Baba Mtakatifu huko Vatican
Kutokana na uongozi wake mzuri Jumuiya ya Kristo ilimteua Bergoglio kiongozi toka mwaka 1973 hadi 1979, mwaka 1980 alihamishwa na kuwa Rector katika Seminary ya San Miguel ambako alisomea pia . alihudumu katika Seminari hiyo hadi mwaka 1986

Bergoglio alipata daraja la Askofu mkuu tarehe 28.02.1998 huko Argentina, Papa John Paul wa II alimwita Vatican Askofu huyo mpya tarehe 21.02.2001 na kumpa heshima kuwa Kardinali wa Argentina.


 Kabla ya Kuteuliwa kuwa Baba Mtakatifu, Kardinali George Mario Bergoglio alishika nafasi mbalimbali za uongozi wa kanisa huko Roma na katika nchi yake pia, hivyo uongozi wake ulikubalika kwanzia nchini kwake na hata katika uongozi wa kaniza zima huko Vatican.











Breaking News: The New Pope Elected in Vatican



White Smoke through above the Sistine Chapel
White smoke appeared from the chimney above the Sistine Chapel, and bells from St. Peter's Basilica have pealed, meaning the 115 Roman Catholic cardinals gathered at the Vatican from all over the world have chosen a new pope. The church's 266th pontiff will replace Benedict XVI, whose surprise resignation last month prompted the cardinals to initiate a conclave, a Latin phrase meaning "with a key," to pick a new leader for the world's almost 2 billion Catholics.

Some of the Pastoric wears for the pope
Although it's not immediately clear who received the necessary two-thirds vote, several candidates were mentioned as front runners, including what could be the first African pope or the first pope from the U.S. or Canada. The new church leader takes over an organization many say is in crisis, from damaging allegations of internal squabbling to the cover-up and abetting of sexual abuse, though the latter issue came to light before Benedict's papacy. Some sources say the Catholic Church in the U.S. has paid out as much as $3 billion to settle sexual abuse claims, though others estimate a billion less. At least eight U.S. Catholic dioceses declared bankruptcy protection. Benedict said in a 1998 U.S. visit that he was ashamed of the sex abuse scandal, and assured that the church would not allow pedophiles to become priests.

The Pope Emeritus also faced criticism for his role in overseeing the church's reaction to the sexual abuse crisis, as well as revelations from the "Vatileaks" incident. The pope's butler was implicated in the leaking of documents that included what Italian media first characterized as evidence of blackmail and disarray among church leaders regarding how to address growing concerns about money laundering.

Shoes for the Pope
 Though Benedict basically dismissed those allegations as exaggerated, he remarked that the leaks and results of the ensuing investigation he commissioned had saddened him. Church outsiders have speculated that the results of Benedict's investigation may have led to his decision to resign from the papacy, a move unprecedented in six centuries.

The new pope will also face pressure to modernize the church on issues from reforming the clergy to allowing contraception. It's unclear if the cardinals will pick a pope who will change the church or a conservative leader who will remain dedicated to its current principals.

Thursday, March 7, 2013

WANAFUNZI 1,000 WASOMEA CHINI MPANDA


ZAIDI ya wanafunzi 1,000 wa Shule ya Msingi Mbugani, iliyopo Kata ya Kakese katika Halmashauri ya mji wa Mpanda wanasomea chini kutokana na ukosefu wa madawati unaoikabili shule hiyo.

Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Anthony Mbawa, alitoa taarifa hiyo jana kwa waandishi wa habari waliotembelea shule hiyo kwa lengo la kuangalia changamoto zinazoikabili shule hiyo.

Alisema shule hiyo ina wanafunzi 1,333 kati yao, 162 ndio wanaosoma wakiwa wamekaa kwenye madawati ambao wanasoma darasa la saba na la sita.

Alisema shule hiyo iliyoanzishwa mwaka 2002, ina madawati 54 kwa shule nzima.
Alieleza changamoto nyingine zinazoikabili shule hiyo kuwa ni mrundikano wa wanafunzi katika madarasa kutokana na uchache wa majengo ya madarasa.

Alitoa mfano kwa wanafunzi wanaosoma darasa la kwanza kwa kueleza kuwa lina wanafunzi 218 wanaosoma kwa wakati mmoja, hali ambayo inasababisha mwalimu kupata shida ya kutoa maelekezo kwa kila mwanafunzi.

Naye mwanafunzi wa darasa la nne, Jafe Thomas, alisema kitendo cha wao kusoma wakiwa wamekaa chini kunafanya washindwe kuandika vizuri.

Pia alisema sare zao zimekuwa zikichafuka kutokana na uchafu wa vumbi unaozagaa chini ya sakafu kwenye madarasa.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji wa Mpanda, Enock Gwambasa, alisema katika kukabiliana na tatizo hilo, Benki ya NMB Tawi la Mpanda imetoa ahadi ya kutengeneza madawati 100 yenye thamani ya sh milioni 15 kwa ajili ya shule hiyo.

Tanzania daima 
 

Monday, March 4, 2013

Mauaji siku ya kupiga kura Kenya


Mmoja wa wale waliojeruhiwa
 Taarifa ambazo bado hazijathibitishwa zinasema kuwa watu 10, wakiwemo maafisa wa polisi wawili, wameuawa mjini Mombasa, Pwani ya Kenya. Tukio hilo lilitokea alfajiri, kuamkia leo wakenya wanapopiga kura.
 
Hata hivyo polisi walithibitisha vifo vya maafisa wao wawili vilivyotokea wakati polisi walipowapiga risasi washambulizi waliokuwa wamejihami kwa mapanga. Lilikuwa shambulizi la kulipiza kisasi.
 
Washambulizi hao wanashukiwa kuwa wafuasi wa kundi la Pwani la Mombasa Republican Army (MRC) ambao wamekuwa wakipigania uhuru wa jimbo la Pwani.
 
Mwandishi wa BBC, Karen Allen, anasema polisi waliweza kuthibitisha vifo vya wanne katika eneo la Changamwe, naye Hassan Majid aliona mtu mmoja kauawa eneo la Mishomoroni. Mwtu mwingine Moja ya miili hiyo ilikuwa imekatwakatwa.
 
Zaidi ya watu 1,000 waliuawa miaka mitano iliyopita katika ghasia zilizotokea baada ya uchaguzi wa mwaka 2007.

MBOWE “AICHANA” SERIKALI MJINI MPANDA


  •   Asema kuhutubia mkutano bila kuitaja CCM au Viongozi wake  ni sawa na Kuhubiri injili bila kumtaja Shetani.
  • Tatizo la Udini liliasisiwa na CCM
  • Alia na janga la Elimu, asema ni bomu tusiloweza kulicontrol
  • Asisitiza serikali bila presha haiendi, mawaziri wa Elimu sharti wawajibike kwa matokeo mabaya ya kidato cha nne
  •  Asuluhisha Mgogoro uliokuwa ukifukuta ndani ya Chama

Freeman Mbowe na Said Arfi wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara  
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Freeman Aikael Mbowe jana amefanya mkutano wa hadhara katika viwanja vya Kashaulili mjini Mpanda ambapo mamia ya wakazi walihudhuria.

Akihutubia mkutano huo Mbowe alizungumzia masuala kadhaa ya kitaifa na kichama likiwemo suala la Askari polisi wa Tanzania, akisifu kazi yao katika Wilaya ya Mpanda kuwa wanafanya kazi kwa maadili na kuwataka Polisi sehemu nyingine Tanzania kuiga mfano wa Polisi Mpanda, akiwapongeza polisi hao amewaahidi kuwa CHADEMA ikishika Dola mwaka 2015 itakuwa pamoja nao.

Mbowe akizindua Harambee ya Ujenzi wa Ofisi ya Chama Mkoa
Katika mkutano huo ambao ulihudhuriwa pia na Viongozi wengine wa CHADEMA Mkoa na wilaya aliwataka wananchi kuipa nafasi CHADEMA kushika Dola mwaka 2015 na wakipime kwa utendaji kazi wake, iwapo wakishindwa basi “wakipige chini” na kuchagua chama kingine, “Biashara ya kufunga ndoa na chama cha siasa ni wendawazimu” alisema Mbowe. Akirejea maneno ya Mwalimu Nyerere  akisema CCM imepoteza mwelekeo, inanuka Rushwa.

Mbowe pia aliwataka vijana na jamii yote kuacha woga na kuchukua hatua ili kulinusuru taifa, kwani Serikali ya sasa bila Presha haiendi, akikumbushia suala la katiba Mpya Alisema Serikali isingekubali kuanza mchakato wa kuandika Katiba mpya kama isingetiwa Presha ndani na Nje ya Bunge.

Viongozi wa BAVICHA katika picha ya pamoja baada ya Mkutano
Akizungumzia tatizo na visa vya udini vinavyoendelea nchini, Mbowe amesema hayo ni matunda ya siasa za kibaguzi zilizoasisiwa na Chama Cha Mapinduzi, akifafanua kauli yake hiyo Mbowe amesema Mwaka 2000 CUF ilikuwa na nguvu na kuwa tishio kwa CCM, hivyo baada ya kuona Viongozi wa CUF wengi ni waislamu walitumia kigezo hicho kuwagawa wananchi kuwa wasichague CUF kwa kuwa ni chama cha Waislamu, amesema kitu hicho kilijenga ufa miongoni mwa jamii huku CCM wakifurahia ushindi, amesema pia kuwa baada ya kuona CHADEMA imekuja juu na kuwa tishio wanatumia mbinu ya Kuwagawa wananchi wakisema kuwa CHADEMA ni chama cha Kikristo, bila kujua wanaendeleza ufa waliokwisha utengeneza awali, hivyo matukio yanayotokea ni zao lililopandwa na CCM wenyewe hivyo hawana budi kulinywa.

Amesema CHADEMA hawachagui mtu kutokana na dini au kabila lake bali utendaji kazi na nia yake ya dhati ya kuihudumia jamii yake. Amesema katika ngazi ya CHADEMA Taifa yenye viongozi sita wanne kati yao ni Waislamu hivyo si sahihi kusema CHADEMA ni chama cha Kikristo, na pia si sahihi kusema CHADEMA ni chama cha Wachaga kwani katika uongozi wa Juu Mchagga ni Mbowe pekee, viongozi wengine wametoka katika makabila mbalimbali nchini.

Kabla ya Mkutano huo wa hadhara wa jana Mbowe alikuwa na kikao cha Ndani na Viongozi wa 
Mbowe akisalimiana na Mkazi wa Mpanda baada ya Mkutano
Chama Mkoa ambapo alisuluhisha migongano iliyokuwa imeanza kukitafuna chama, na katika mkutano wa hadhara Mbowe aliwasimamisha viongozi mbalimbali ambao kwa namna moja ama nyingine walihusika katika mgogoro huo nao walikiri hadharani kuacha tofauti zao na kuwa kitu kimoja na kufanya kazi kwa pamoja kwa maslahi ya Chama na Taifa kwa ujumla.

Katika Mkutano huo Mbowe aliongoza Harambee maalumu kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi ya Chama Mkoa ambao unapaswa kukamilika ndani ya mwaka mmoja. Katika harambee hiyo Mbowe aliahidi kuchangia Tsh. 5,000,000/- Wabunge wa CHADEMA waliahidi Mchango wa Tsh.1,500,000/= kila mmoja kwa ajili ya kununua kiwanja itakapojengwa ofisi. Katika harambee hiyo jumla ya fedha iliyochangwa ilikuwa Tsh. Milioni Kumi 10,000,000/= huku Fedha Taslimu zikipatikana Tsh. 200,000/=

Picha Zote na Khalfan Zozi

Friday, March 1, 2013

CHADEMA KUUNGURUMA MPANDA

  • Viongozi wa Kitaifa Kuhutubia.
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kinatarajia kufanya Mkutano Mkubwa siku ya Jumamosi ya Tarehe 02/03/2013 katika viwanja vya Kashaulili mjini Mpanda.

Taarifa za kuaminika kutoka kwa Katibu wa BAVICHA wilaya ya Mpanda Bwana Khalfan Zozi, alizozituma katika Mtandao wa CHADEMA Mkoani Katavi zinasema kuwa katika Mkutano huo, mambo mbalimbali ya Kitaifa yatazungumzwa na Viongozi hao wa CHADEMA Taifa.

Uongozi wa CHADEMA Mpanda Umewahamasisha wakazi wote wa Mpanda Mjini na Viunga vyake bila kujali itikadi za kisiasa kujitokeza katika viwanja vya Kashaulili ili waweze kusikia viongozi wa kitaifa wanasemaje na kufahamu msimamo wa CHADEMA kuhusu masuala mbalimbali yanayoendelea katika taifa kwa sasa.

Viongozi wanaotarajiwa kuhutubia Mkutano huo ni Freeman Aikael Mbowe (Mwenyekiti Taifa), Said Amour Arfi (Makamu Mwenyekiti Taifa) na Godbless Lema (Mbunge wa Arusha Mjini)

Akitoa ufafanuzi kuhusu Mkutano huo wa Jumamosi 02/03/2013 Bwana Zozi amesema mkutano huo pamoja na mambo mengine utahusu maandalizi ya awali uzinduzi wa kanda maalumu ya kichama (Kanda za Ziwa Tanganyika) ambayo itahusisha mikoa ya Katavi, Rukwa na Kigoma, pia amesema kuwa mkutano unalenga kujenga chama zaidi katika kuelekea Uchaguzi mkuu ujao.

CHADEMA kimekuwa ni chama kinachokua na kuungwa mkono na raia wengi kutokana na kufanya mikutano na kuwafikia wananchi wengi zaidi wakijipambanua kuhusu masuala mbalimbali ya kitaifa kupitia harakati mbalimbali kama Operation Sangara, na Movement For Change (M4C) ambazo zimesaidia kuondoa dhana kuwa Vyama vya Upinzani ni vyama vya Msimu vinavyoibuka kipindi cha uchaguzi na kupotea uchaguzi ukiisha.

KATAVI UP2DATE inawatakia mafanikio CHADEMA katika mkutano huo wa kesho Jumamosi tarehe 02.03.2013 uweze kufanyika na kumalizika salama.

Wednesday, February 27, 2013

FIDIA YA TSH.300/= KUWAONDOA WAKAZI MPANDA HOTELI?

    • Ni zoezi linalohusisha kubomoa makazi ya Raia kupisha Upanuzi wa Barabara

    • Inasemekana walishalipwa fidia Mwaka 1930 ya Tsh.300/=

      Wakazi walia, wasema Barabara iliwakuta

      RC awataka raia wapoe kusubiri maamuzi ya Mahakama

Polisi Mpanda wapiga marufuku maandamano ya wananchi

JESHI la Polisi Mkoa wa Katavi limepiga maarufu maandamano ya wananchi wa mitaa ya Misunkumilo na Mpanda hoteli waliopanga kuandamana kutaka Meneja wa TanRoads Mkoa wa Katavi, Izack Kamwelwe aondolewe.

Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Joseph Myovela alisema wanachi hao waliomba kibali cha kuwaruhusu waandamane Februari 25 mwaka huu.

Wananchi waliomba kufanya maandamano hayo baada ya Tanroads kuwataka baadhi ya wakazi wa mitaa hiyo wahame kupisha upanuzi wa barabara ya kutoka Mpanda kwenda Uvinza mkoani Kigoma.

Katika upanuzi huo nyumba za wanachi hao zitakazobomolewa hazitalipwa fidia yoyote kwa kile kinachodaiwa kuwa walishakwisha kulipwa fidia mwaka 1932 Katika malipo hayo kila mwanachi wa maeneo hayo alilipwa na serikali ya mkoloni Sh 300 kama fidia ya kuhamishwa kwenye maeneo hayo.

Wananchi hao wanadai malipo hayo yalikuwa ni kwa ajiri ya kupisha uchimbaji wa dhahabu na siyo kupisha ujenzi wa barabara.

Madai mengine ya wananchi hao ni kuwa ujenzi wa barabara hiyo umewakuta wakiwa tayari wanaishi kwenye maeneo hayo kwa zaidi ya miaka 70 na wamezeekea hapo.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Dk. Rajabu Rutengwe akiwa na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa, alikuwa na mkutano wa hadhara na wananchi wa mitaa hiyo katika shule ya msingi Misunkumilo na kuwaeleza kuwa suala hilo tayari lipo mahakamani hivyo ni vizuri wakasubiri uamuzi wa mahakama.

Tuesday, February 26, 2013

Utafiti wa Synovate: Slaa awaburuta wenzake Mbio za Urais 2015

  • Pinda Amfukuzia (atoshana nguvu na Zitto)
  • Wengine wasindikiza kwa mbali
  • Umaarufu wa CCM waongezeka kiduchu
WAKATI baadhi ya wanasiasa wakiwa wameanza kujiwinda kwa ajili ya kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2015, Shirika la Utafiti la Synovate limetoa matokeo ya utafiti wake ambao unaonyesha vigogo tisa kuwamo katika mchuano huo.
Utafiti huo umeonyesha kuwa endapo uchaguzi huo ungefanyika sasa, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willibrod Slaa angeibuka mshindi baada ya kuongoza orodha hiyo akipata asilimia 17.
Dr.Wilbrod Slaa

Katika matokeo ya utafiti huo uliofanywa Desemba mwaka jana, Dk Slaa anafuatiwa kwa mbali na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ambaye amefungana na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe kila mmoja akipata asilimia tisa.

Hata hivyo, licha ya kuongoza, Dk Slaa ameporomoka kwa asilimia 25 ikilinganishwa na matokeo ya utafiti kama huo uliofanywa na taasisi hiyo mwaka 2011 ambapo alipata asilimia 42.

Kadhalika, umaarufu wa Pinda ambaye anaongoza miongoni mwa wagombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), umeshuka kwa asilimia tatu kutoka 12 za mwaka juzi, wakati Zitto ameendelea na kiwango kilekile cha asilimia tisa alizopata katika utafiti uliotangulia.
Wengine wanaofuata na asilimia walizopata kwenye mabano ni Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli (8), Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa (7) na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba (5).

Pia wamo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe (4) ambaye amefungana na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe (4) na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta (2).

Ikilinganishwa na utafiti wa 2011, Lipumba ameporomoka kwa asilimia tisa.
Lowassa amepanda kwa asilimia sita, Dk Magufuli asilimia nne, Mbowe na Membe wamepanda kwa asilimia mbili kila mmoja, wakati Sitta amebaki katika kiwango kilekile cha asilimia mbili.

Hata hivyo, utafiti huo umeonyesha kuwa wananchi ambao hawana uamuzi wa kuchagua mtu yeyote kati ya hao kwa sasa ni asilimia 18, likiwa ni ongezeko la asilimia 12 ikilinganishwa na utafiti uliotangulia.

CCM yatamba

Katika utafiti huo, CCM kimeonyesha kuwa ni chama ambacho asilimia 52 ya wananchi wangependa kujiunga nacho, kikiwa kimepanda chati kwa asilimia moja kutoka asilimia 51 mwaka jana.

Kwa upande wa Chadema, wananchi ambao wanapenda kujiunga nacho imeshuka kutoka asilimia 35 mwaka 2011 hadi 31 mwaka jana.

Uwezekano mkubwa wa CCM kupanda chati ni kutokana na ukweli kuwa mwaka jana kilikuwa na uchaguzi ulioanzia ngazi ya mashina hadi taifa na kuibua vuguvugu kubwa masikioni mwa wananchi.

Chadema hakikuwa na harakati kubwa za kisiasa ukiacha kampeni ya Movement For Change (M4C), ambayo kwa kiasi haikuwa na pilika kama uchaguzi wa CCM.
Chama kingine ni CUF ambacho kimeporomoka kwa kupata asilimia 10 mwaka 2011 hadi nne mwaka 2012.

Hata hivyo, asilimia ya wananchi kutokutaka kujihusisha na chama chochote imepanda kutoka asilimia mbili mwaka 2011 hadi 12 mwaka 2012.

Source: www.mwananchi.co.tz

Saturday, February 23, 2013

Mengine Yajiri Zanzibar!

Taarifa zilizopo ni kuwa mtu mmoja anayeitwa Ali Khamis ambaye ni Imamu wa Msikiti Mkaazi wa Mwakaje amepigwa mapanga na watu wasiojulikana huko Kidoto Mkoa wa Kaskazini Unguja jana,

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, Ahmada Khamis amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambalo anasema limetokea majira ya saa 8 mchana huko Kitope wakati Marehemu akiwa shambani kwake,

Kwa mujibu wa taarifa za polisi zinasema Imamu huyo alipigwa mapanga shingoni kwake na kupoteza damu na kusababisha kifo chake wakati akikimbizwa hospitali.

Jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.

IJUE SIRI YA NEMBO YA TAIFA:

  • Ilitokana na  Tambiko kabla Mwalimu kushika Nchi
  • Liliaandaliwa na Chief Fundikira wa Tabora
  • Binti Kamba, Mwanamke shujaa aliyeko katika nembo ya Taifa.
  • Alimtwanga kofi Mzungu kuokoa maisha ya Nyerere na wana TANU
  • Unajua Binti Kamba yuko wapi sasa?


MFAHAMU BINTI KAMBA:

Anaanza kwa kusema: “Nilijiunga na siasa nikiwa na umri wa miaka 18 tu, nilikuwa bado kigori,’
Anasema harakati za siasa wakati huo zilianza kushika kasi huku zikiendeshwa na wanaume pekee. Baadaye kukatokea haja ya kuwashirikisha wanawake.

Kwa sababu hiyo anasema  alifuatwa ili ajiunge  katika ulingo wa siasa, lakini haikuwa kazi rahisi kujiunga baada ya kukatazwa na walezi wake.
Alipokataa anasema akafuatwa mwanamke mwingine aliyeitwa Tatu Mzee, ambaye alipopelekwa kwa waasisi wa siasa, hakuweza  kuzungumza kwani alijawa na aibu.
Kura nyingine iliangukia kwa marehemu Bibi Titi Mohamed ambaye wakati huo alikuwa mwimbaji mahiri katika harusi na sherehe za jando na unyago.
“Bibi Titi alipopelekwa mbele ya waasisi wa TANU, alizungumza kwa umahiri na alipata kura zote,” anasema
Bibi Titi alikuwa ni mwanamke wa kwanza  kuingia katika siasa hata kabla chama cha TANU hakijazaliwa.
Binti Kamba akiwa nyumbani kwake anakougulia

Mkutano wa kwanza wa watu weusi
Mkutano wa kwanza wa chama ulifanyika mwaka   1952.  Maelfu ya Watanganyika walifurika, akiwemo Binti Kamba  ili kusikia walichotaka kukisema Watanganyika wenzao.
Anasema  maajabu ya kwanza ya Mwalimu Nyerere yalijionyesha siku hiyo  mara baada ya wingu la mvua kubwa na la ajabu kutanda angani dakika chache kabla mkutano haujaanza.
“Mwalimu  alikuwa na kitu cha kipekee pengine ndio maana wengine walimwita mchawi. Mkutano wake wa kwanza ulikuwa na miujiza,” anasema
Anasimulia zaidi na kusema kuwa, wahudhuriaji waliokuwa wamebeba miamvuli kwa ajili ya kujilinda na jua, walianza kuitumia kujilinda kwa ajili ya mvua iliyoanza kudondosha manyunyu.
Anasema: “Mara baada ya Nyerere kupanda jukwaani, aliwaambia Watanganyika washushe miamvuli na wala wasijifunike kwani mvua hiyo haitanyesha,” anasema na kuongeza:
“Watu walishusha miamvuli, wingu lilipotea na mkutano ukapamba moto. Basi tangu siku ile watu walianza kumfananisha Nyerere  na nabii.”
Binti Kamba  baada ya kusikia  sera za Nyerere kwa mara ya kwanza na kuuona ushupavu aliokuwa nao, hakusita kujiunga na siasa mara moja, akiwa ni mwanamke wa pili kuingia katika chama.
“Nilikata kadi yangu ya uanachama siku ile ile kwa shilingi mbili tu nikiwa mwanamke wa kwanza katika chama cha vijana(TYL) kilichoongozwa na Joseph Nyerere na mwanamke wa pili katika TANU” anasema
Anasema, wakati ule kila mmoja alikuwa na mapenzi na chama, wote walikuwa na nia moja na walipumua pumzi moja tu, nayo ni uhuru.
Ampiga kofi mzungu
Mwasisi huyu mkakamavu licha ya kuwa umri umeshamtupa mkono, anasema miongoni mwa mambo yaliyompatia sifa ni pale alipompiga askari wa Kiingereza kofi.
Anasimulia mwanzo wa tukio hilo na kusema kuwa  baada ya kufukuzwa katika ofisi yao ya awali ya chama iliyokuwa mtaa wa Livingstone Kariakoo, walipata eneo ulipo Uwanja wa Taifa sasa.
“Eneo hilo lilikuwa ni pori lenye miba na miti mirefu migumu. Tukiwa vijana wa chama wenye ari na nguvu, tulisafisha kwa mikono yetu na kuanza kujenga ofisi,”anasema
Anasema baada ya ofisi kujengwa na eneo la kufanyia mikutano kujengwa pia, njama za wakoloni za kutaka kuwapoteza zilionekana waziwazi.
“Tuligundua siri nzito iliyofanywa na Serikali ya Kiingereza. Walitegesha baruti na mafuta petroli karibu na jukwaa ili watulipue. Lakini sisi kama mabinti warembo enzi zile, tulitumia uanamke wetu na tuliijua siri ile,” anasema Binti Kamba akicheka kwa fahari
 Anasema walipokwenda kumweleza Nyerere siri ile, alipanga mikakati mizito ya ulinzi ikiwamo kuwatahadharisha wanachama na wananchi wengine kutovuta sigara au kutupa kitu chochote chenye moto katika eneo lile.
“Mimi, Simkoko na Lumumba tulikuwa kwenye jeshi la ulinzi, tuliwekwa katika milango minne ya jengo lile ili kulinda usalama, wakati mkutano ukiendelea,” anasema
Anasema akiwa amesimama mlango wa mbele wa ofisi hiyo, alimuona Mwingereza akija kwa kunyata katika ofisi ile, kisha akawasha sigara na kuanza kuvuta.
“Kwa hofu nilimrukia na kumzaba kofi kali kwani nilijua kabisa kuwa akitupa sigara ile katika eneo lenye baruti au petroli, basi tutaungua wote,” anasema
Anasema kwa kuwa alikuwa hafahamu lugha ya Kiingereza, alimwambia Mwingereza huyo   “no speaker hapa” akiwa na maana ya “no smoking here”yaani usivute sigara hapa.
Kitendo chake cha kuthubutu kumwadhibu mkoloni aliyeogopewa kwa ajili ya taifa lake anasema kilimpa heshima kwa wanachama wengine.
Anasema baada ya hapo mkutano uliendelea na harakati za kudai uhuru zilishika kasi siku hadi siku.
 Tambiko na chanzo cha nembo ya uhuru na umoja
Anaeleza kuwa yeye Binti Kamba  na marehemu Juma(mwasisi wa TANU)  ndiyo walioko katika picha ya nembo ya Uhuru na Umoja.
Chanzo cha picha ile kilikuwa ni tambiko maalum kwa ajili ya Nyerere  mara baada ya wakoloni kumpa cheo cha Uwaziri Mkuu.
Mwasisi huyu wa TANU anasema baada tu ya wazee wa wakati ule  kusikia kuwa Waingereza wamempa Nyerere cheo hicho, Chifu Fundikira alitoka Tabora na kuja Dar es Salaam  kumsihi Nyerere afanye tambiko kabla ya kuanza kazi.
“Ilikuwa ni lazima tumfanyie tambiko kwa sababu tulijua kuwa wakoloni wana yao na walitaka kumrubuni Nyerere kwa  cheo, ili asahau harakati za kupigania  uhuru,” anasema
Tambiko hilo lilikuwa ni pamoja na unga maalum uliokuwa ndani ya kibuyu, ngao na pembe za ndovu. Kibuyu hicho nje kilikuwa na picha ya sura ya mtu
“Wazee kadhaa akiwemo Chifu Fundikira walikuwa wakichukua unga kutoka katika kibuyu hicho na kummwagia mwalimu  pamoja na mke wake usoni,” anasema
Anasema hawakutakiwa kuingia ndani ya nyumba yao mpya au ofisi bila kufanyiwa tambiko hilo.
 
“Wakati wa kufanywa kwa tambiko lile, mwalimu na mke wake walitakiwa wakae nyuma ya ngao na pembe za ndovu zikae kulia na kushoto kwao,” anasema
Anasema kwa kuwa yeye na Juma walikuwa ndiyo vijana wenye nguvu ilibidi wateuliwe kuzishika pembe hizo,  huku Mwalimu
Nyerere pamoja na mke wake wakiwa nyuma ya ngao hiyo, ngao na pembe vyote vilisimamishwa kama vinavyoonekana katika nembo.
Hata hivyo, Binti Kamba  ambaye hakuwahi kuwa na mtoto katika maisha yake anaongeza kuwa  ngao na pembe zile zilikuwa na siri nzito ambayo katu hawezi kuisema.
“Mwanachama wa TANU anatakiwa kutunza siri na si mropokaji, nimekula kiapo sitofanya hivyo” anasema
Anasema picha ya nembo ya uhuru na umoja haikuwahi kupigwa kwa kutumia kamera bali ilichorwa kutokana na tukio hilo la tambiko na kuongezewa mchoro wa mlima Kilimanjaro na maneno yanayosomeka ‘Uhuru na Umoja’

Maisha ya sasa
Hivi sasa mwasisi huyo yupo taabani kitandani. Maradhi hasa ya miguu yamemwandama, huku akilia kukosa uwezo wa fedha kukidhi mahitaji yake mbalimbali.
Anadai kuwa wanachama wa CCM wa sasa wamemsahau na wala  hawajui  umuhimu wake kwa Taifa hili.Anasema wamemtelekeza na kumtupa mithili ya ganda lisilo na thamani tena kwa mlaji.

Imechukuliwa kutoka: http://www.mwananchi.co.tz

 

Thursday, February 21, 2013

Angalia video ya Sheihk akihimiza mauaji ya Mapadre na Maaskofu

Angalia Video hii ya Sheihk Ilunga akihimiza mauaji ya mapadre na maaskofu kisha toa maoni yako.
Toa maoni yako.

Tuesday, February 19, 2013

Dr.Slaa Ahudhuria maziko ya Padre Mushi

Katibu Mkuu wa CHADEMA Taifa leo hii anahudhuria Ibada ya Maziko ya Padre Evaristus Mushi aliyeuawa siku ya Jumapili huko Zazinzibar.

Akiongea na Radio Maria kabla ya Misa kuanza Dr. Slaa ameikumbusha Serikali kukumbuka kazi yake Msingi kwa watu wake ambayo ni kulinda Uhai wa Wananchi wake. Akifafanua kauli hiyo amekumbusha matukio kadhaa ya mauaji na mashambulizi yaliyojitokeza hivi karibuni ambayo hadi sasa Serikali haijachukua hatua zozote. amekumbusha matukio ya Padre kunusurika kifo baada ya kupigwa Risasi hapo hapo Zanzibar siku  za karibuni, tukio la vurugu za Geita zilizosababisha mauaji ya Mchungaji na Matukio ya Katibu wa Mufti kumwagiwa Tindikali huko Zanzibar.

Pia Slaa ambaye aliwahi kuwa Padre ametoa ufafanuzi wa Kihistoria kuwa  Msingi wa Ukristo TAnzania ni Zanzibar kwani Wamisionari wa Kwanza kuingia Afrika Mashariki walianzia Visiwani humo kabla ya kwenda sehemu nyingine,  hivyo Kuna ulazima wa kuangalia kwa nini mauaji na Visa vizidi katika kipindi hiki.

Ameikumbusha pia Serikali kufuatilia kiini cha matukio hayo ya mauaji  na si kuishia katika kuangalia au kujiuliza juu ya matunda ya mambo ambayo yana msingi wake.


Misa hiyo ya imeongozwa na Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, na kuhudhuriwa pamoja na viongozi Mbalimbali wa kisiasa, serikali na Dini mbalimbali.