Wednesday, February 27, 2013

FIDIA YA TSH.300/= KUWAONDOA WAKAZI MPANDA HOTELI?

    • Ni zoezi linalohusisha kubomoa makazi ya Raia kupisha Upanuzi wa Barabara

    • Inasemekana walishalipwa fidia Mwaka 1930 ya Tsh.300/=

      Wakazi walia, wasema Barabara iliwakuta

      RC awataka raia wapoe kusubiri maamuzi ya Mahakama

Polisi Mpanda wapiga marufuku maandamano ya wananchi

JESHI la Polisi Mkoa wa Katavi limepiga maarufu maandamano ya wananchi wa mitaa ya Misunkumilo na Mpanda hoteli waliopanga kuandamana kutaka Meneja wa TanRoads Mkoa wa Katavi, Izack Kamwelwe aondolewe.

Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Joseph Myovela alisema wanachi hao waliomba kibali cha kuwaruhusu waandamane Februari 25 mwaka huu.

Wananchi waliomba kufanya maandamano hayo baada ya Tanroads kuwataka baadhi ya wakazi wa mitaa hiyo wahame kupisha upanuzi wa barabara ya kutoka Mpanda kwenda Uvinza mkoani Kigoma.

Katika upanuzi huo nyumba za wanachi hao zitakazobomolewa hazitalipwa fidia yoyote kwa kile kinachodaiwa kuwa walishakwisha kulipwa fidia mwaka 1932 Katika malipo hayo kila mwanachi wa maeneo hayo alilipwa na serikali ya mkoloni Sh 300 kama fidia ya kuhamishwa kwenye maeneo hayo.

Wananchi hao wanadai malipo hayo yalikuwa ni kwa ajiri ya kupisha uchimbaji wa dhahabu na siyo kupisha ujenzi wa barabara.

Madai mengine ya wananchi hao ni kuwa ujenzi wa barabara hiyo umewakuta wakiwa tayari wanaishi kwenye maeneo hayo kwa zaidi ya miaka 70 na wamezeekea hapo.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Dk. Rajabu Rutengwe akiwa na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa, alikuwa na mkutano wa hadhara na wananchi wa mitaa hiyo katika shule ya msingi Misunkumilo na kuwaeleza kuwa suala hilo tayari lipo mahakamani hivyo ni vizuri wakasubiri uamuzi wa mahakama.

No comments:

Post a Comment