Saturday, April 6, 2013

BABU WA SAMUNGE AJA KIVINGINE

  • Adai kugundua unyayo wa mtu wa 182 baada ya Adam na Hawa
Mch. Ambilikile Mwasapile
MCHUNGAJI Ambilikile Mwasapile (78) ameibuka na kudai Mungu amemuonyesha unyayo wa mtu wa 182 tangu kuumbwa kwa Adamu. Masapila amekuwa maarufu kwa kutoa huduma ya dawa kwenye kikombe iliyodaiwa kutibu magonjwa sugu. Maelfu ya watu walikwenda kunywa “kikombe hicho cha Babu” mwaka juzi.

Akiwa ametanguliza sharti la kutopiga picha unyayo huo ulio kwenye jiwe alilolihifadhi nyumbani kwake, Masapila aliwaambia waandishi wa habari kuwa Mungu anaendelea kumuonyesha miujiza mingine.

“Nimepata unyayo wa mtu wa kale na Mungu ameniambia mtu huyo ni wa 182 tangu uumbaji wa Adamu na alikuwa binti anayeitwa Tutali.

“Tutali alikanyaga jiwe likazama kama mnavyoona huu ni unyayo wake… awali Mungu alinionyesha mahali ulipokuwa na akanielekeza nikaenda kuuchukua.

“Lakini mpaka sasa bado hajazungumza na mimi kwa ajili ya kuuweka hadharani hatua hiyo ni mpaka Mungu atakaponiruhusu,” alidai Masapila.

Alipoulizwa kama amewasiliana na wanasayansi waukague na kujiridhisha kama ni unyayo kweli, alisema hajafanya hivyo kwa vile anaendelea kumsikiliza Mungu.

“Hamfahamu bustani ya Eden ilikuwa kwenye hili eneo la Ngorongoro.

Niwaombe Watanzania waendelee kusubiri na wenye nia mbaya wataona maajabu zaidi,” alisema Masapila.

Akifafanua kuhusu huduma yake kupungukiwa na watu, Masapila alisema, mambo mengi yalichangia ikiwamo gharama za kufika nyumbani kwake kunywa dawa.

No comments:

Post a Comment