Sunday, December 8, 2013

DR. SLAA APOPOLEWA MAWE KASURU KIGOMA

Katika hali ya kushangaza wanaojiita wafuasi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wamemrushia Mawe Katibu Mkuu wa Chama hicho wakati akihutubia mkutano wa chama mjini Kasuru.
Vijana hao wapatao kumi na tano waliokuwa na mabango yenye mbalimbali kama vile "Zit to kwanza Chadema baadae" walianza kumrushia mawe hali iliyopelekea askari Polisi kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) kumnusuru na kumficha sehemu ambayo mpaka tunakwenda mitamboni haikujulikana alipo.
Aidha polisi walitumia mabomu ya machozi kuwatawanya wafanya furugu hao hali iliyopelekea mkutano kuvunjika.
Katavi Up To Date inaendelea KufAnya utafiti wa chanzo cha vurugu hizo na wahusika wake...itaendelea kuwajuza kadri taarifa zitakavyokuwa zinapatika.


Posted via Blogaway

No comments:

Post a Comment