Thursday, March 28, 2013

MIAKA 30 JELA KWA UBAKAJI

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi ya Wilaya ya Mpanda, Mkoa wa Katavi, imemhukumu Pascal Fransisi (20) mkazi wa kijiji cha Igalula, kifungo cha miaka 30 jela, baada ya kupatikana na hatia ya kubaka mwanamke.

Hukumu hiyo, ilitolewa hapo jana na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda, Chiganga Tengwa, baada ya kuridhika na ushahidi wa mashitaka uliotolewa mahakamani hapo.

Awali mwendesha mashitaka, Ally Mbwijo, alidai mshitakiwa alitenda kosa hilo Februari 11, mwaka huu, saa 10 jioni nyumbani kwake.

Alidai siku hiyo, Fransins akiwa nyumbani kwake alimbaka mwanamke (jina tunalo) mkazi wa kijiji cha Kambanga, wakati akiwa anapita karibu na nyumbani kwake.

Alidai pamoja na mwanamke huyo kumkatalia kuingia ndani kwake, Fransis aliweza kufanikiwa kumwingiza ndani ya nyumba yake kwa nguvu.

Mshitakiwa baada ya kumwingiza ndani ya nyumba yake, alianza kumwingilia kwa nguvu kimwili, licha ya mwanamke huyo kupiga kelele za kuomba msaada.

Hakimu Chiganga, baada ya kusikiliza maelezo ya upande wa mashitaka na mshitakiwa aliridhika na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na ndipo alipomtaka mshitakiwa ajitetee kutokana na mahakama kumwona ana hatia.

Mshitakiwa Fransis katika utetezi wake, aliiomba mahakama isimpe adhabu kutokana na kile alichokieleza kuwa mwanamke huyo walikuwa na mahusiano naye ya kimapenzi.

Alidai mwanamke huyo aliamua kumshitaki baada ya kuwa wamemaliza tendo la ndoa na Fransis kushindwa kulipa fedha walizokubaliana.

Hakimu Chiganga, aliiambia mahakama kuwa mshitakiwa amevunja sheria ya kifungu namba 30 na 31 cha Kanuni ya Adhabu ya Marekebisho ya Sheria ya Mwaka 2002,

kwa hali hiyo mahakama imemtia hatiani, hivyo imemhukumu Fransis kwenda jela miaka 30 jela.

Wednesday, March 27, 2013

KATAVI NATIONAL PARK: How to reach and Enjoy the Park

Park regulations

Park rules and regulations

  • Plan your journey! Start your trip early because you must be back in the camp by 7 pm.
  • Unless you are specifically allowed to drive off-road, stay on the roads and tracks in all parts of the park. No game drives in the wilderness areas!
  • Be considerate to wildlife – do not harass, feed or interfere with wildlife. Do not get out of the vehicle when close to any animal!
  • Leave all plants, animals, skulls, bones, rocks or any other objects in the park where they belong.
  • Do not bring live animals or plants into the park.
  • Do not throw seeds of fruits and vegetables into the wild. They could start to grow.
  • Do not start fires unless at authorized camps.
  • Do not throw bottles, plastic bags, food waste from your car into the wild. Please make sure to take your trash with you or dispose it in proper dustbins.
  • Do not waste water.
  • Do not bring any firearms inside the park!
  • For your safety and safety of the wildlife, keep to the 50 km speed limit on all roads including the public roads Mpimbwe and Sumbawanga! Wildlife has the right-of-way everywhere in the National Park!
  • Do not cause any noise or create any disturbance which is likely to disturb other visitors and the animals.
  • Take precautions against malaria.
  • Tsetse biting has not yet caused medical problems in Katavi National Park.
  • Be aware of snakes!

Access

Best time to visit the park

Katavi National Park can be visited all year round. During the drier months (May to October and December to February), the animals congregate around the remaining water bodies and can be reached easily. During the wetter months, the extensive wetlands offer splendid scenery to adventurous visitors.

Location

Katavi National Park is located in Mpanda District, Rukwa Region in Western Tanzania. Currently, the main road that connects Mbeya and Sumbawanga with Mpanda town and Kigoma still crosses the park. The main entrance gate is close to Sitalike village, which is located along that main road 40 km south of the district capital Mpanda and 205 km north of the regional capital Sumbawanga.

Access to Katavi National Park

By air:
  • Fly directly to Katavi: This is the easiest way to reach Katavi at Sitalike or Ikuu airstrips. Another airstrip is available at Mlele
  • Safari Air Link runs the only scheduled flights between Katavi/Mahale to Ruaha, Selous, and Dar es Salaam/Zanzibar (Terminal 1 Julius Nyerere International Airport), P.O. Box 18065, Dar es Salaam, T: +255 777 (or 784) 723274, +255 783 397235, +441 452 862288, flights@flysal.com
  • Fly to Tabora or Kigoma: Regular flights are operated by Precision Air from Dar es Saalam to Tabora and Kigoma. From there you will have to continue by public transport or other arrangements.
By railway:
  • To Tabora and Mpanda: From Dar es Salaam regular trains go to Tabora from Tanzania Central Railways (from where they continue to Kigoma or Mwanza). From there a connection goes to Mpanda. The entire trip requires two travel days.
  • To Mbeya: By Tazara Railway or Bus from Dar es Salaam to Mbeya (Iyunga), then by road using public transport.
By road:
  • By road from Dar es Salaam/Mbeya: Drive to Mbeya in one day, then head to Sumbawanga and Sitalike/Katavi National Park. This is a two to three day safari (17hrs approximately).
  • Take the adventurous route and come by car from Arusha/Tabora: via Babati, Singida, Nzega and Tabora. There are two alternatives: Tabora to Mpanda or Tabora to Inyonga, Mlele and then to Sitalike/Katavi National Park.
  • By road from Kigoma via Uvinza and Mpanda to Katavi National Park.
From/to Mahale: Arrangements can be made from Katavi National Park HQ to go to Mahale National Park through Kabwe - Lukoma - Karema. If you are coming from Mahale National Park the arrangements can be made by the park warden.

Getting around inside the park

Hiring a vehicle is possible at TANAPA. A four-wheel drive car with a driver costs 100 US$ per day for 100 km
If you are driving yourself, you can obtain a map at the headquarters.
Hiring a guide (ranger) to the best places of Katavi is possible at the TANAPA headquarters.
Walking safaris guided by an armed ranger can be arranged.

Human Brain Analysis – Men vs. Women



1. MULTI-TASKING

Women – Multiple process
Womens brains designed to concentrate multiple task at a time.
Women can Watch a TV and Talk over phone and cook.
Men – Single Process
Mens brains designed to concentrate only one work at a time. Men can not watch TV and talk over the phone at the same time. they stop the TV while Talking. They can either watch TV or talk over the phone or cook.

2. LANGUAGE

Women can easily learn many languages. But can not find solutions to problems. Men can not easily learn languages, they can easily solve problems. That’s why in average a 3 years old girl has three times higher vocabulary than a 3 years old boy.

3. ANALYTICAL SKILLS

Mens brains has a lot of space for handling the analytical process. They can analyze and find the solution for a process and design a map of a building easily. But If a complex map is viewed by women, they can not understand it. Women can not understand the details of a map easily, For them it is just a dump of lines on a paper.

4. CAR DRIVING.

While driving a car, mans analytical spaces are used in his brain. He can drive a car fastly. If he sees an object at long distance, immediately his brain classifies the object (bus or van or car) direction and speed of the object and he drives accordingly. Where woman take a long time to recognize the object direction/ speed. Mans single process mind stops the audio in the car (if any), then concentrates only on driving.

5. LYING

When men lie to women face to face, they get caught easily. Womans super natural brain observes facial expression 70%, body language 20% and words coming from the mouth 10%. Mens brain does not have this. Women easily lie to men face to face.
So guys, do not lie face to face.

6. PROBLEMS SOLVING

If a man have a lot of problems, his brain clearly classifies the problems and puts them in individual rooms in the brain and then finds the solution one by one. You can see many guys looking at the sky for a long time. If a woman has a lot of problems, her brain can not classify the problems. she wants some one to hear that. After telling everything to a person she goes happily to bed. She does not worry about the problems being solved or not.

7. WHAT THEY WANT

Men want status, success, solutions, big process, etc… But Women want relationship, friends, family, etc…

8. UNHAPPINESS

If women are unhappy with their relations, they can not concentrate on their work. If men are unhappy with their work, they can not concentrate on the relations.

9. SPEECH

Women use indirect language in speech. But Men use direct language.

10. HANDLING EMOTION

Women talk a lot without thinking. Men act a lot without thinking.

Thursday, March 14, 2013

Mama auawa kwa kucharangwa Mapanga Itenka

MWANAMKE mmoja, Solile Juma (52) mkazi wa Kijiji cha Songambele, Kata ya Itenka, Wilaya ya Mlele mkoani Katavi ameuawa kwa kukatwakatwa mapanga wakati akiwa amelala nyumbani kwake. Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi, Joseph Myovela alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 9.00 usiku nyumbani kwa marehemu ambaye alikuwa akiishi na mwanae wa kike, Nkamba Chambani (15).

Alisema siku hiyo ya tukio Solile alikuwa na mwanae na baada ya kumaliza kula mlo wa usiku waliingia kulala, yeye akilala chumbani na mwanae sebuleni. “Ilipofika muda huo walisikia mlango ukivunjwa kwa kitu kizito na watu wasiofahamika idadi yao kisha kuingia ndani na kumtaka Solile atoe fedha zote alizokuwa nazo, lakini hakuwajibu,” alisema.

 Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda huyo baadaye walimshambulia kwa kumkatakata kwa mapanga sehemu mbalimbali za mwili huku mwanae ambaye walimkataza kupiga mayowe akishuhudia. “Baada ya kuona mama amefariki dunia watu hao walitokomea mahali kusikojulikana huku wakiwa hawajachukua kitu chochote,” alisema mtoto wa marehemu. Mtoto huyo alieleza kwamba baada ya kuona mama yake ameuawa aliendelea kukaa ndani hadi kulipopambazuka ndipo alipokwenda kumtaarifu babu yake, Juma Makoja ambaye naye alitoa taarifa kwa uongozi wa kijiji ambao nao walizitoa polisi.

Katika tukio hilo mtoto huyo hakujeruhiwa sehemu yoyote ile hali ambayo inaashiria kifo hicho kusababishwa na imani za kishirikina. Polisi wameahidi kuendelea na uchuguzi kuwasaka waliohusika na mauaji hayo.

 Source; Tanzania Daima

Wednesday, March 13, 2013

Mfahamu Papa Francisco wa I

George Mario Bergoglio-Papa Fransisco wa Kwanza
Jorge Mario Bergoglio,aliyezaliwa December 17, 1936 ndiye Papa mpya wa Kanisa Katoliki Duniani na Khalifa wa Mtakatifu Petro, amechaguliwa leo Tarehe 13.03.2013  na kuchukua jina la kichungaji la Papa Francico wa Kwanza, kabla ya kuchaguliwa kuwa Papa alikuwa Kardinali wa kanisa Katoliki nchini Argentina, alihudumu kama Askofu Mkuu wa Jimbo la Buenos Aires tangu mwaka 1998 na alipata cheo cha Kardinali mnamo mwaka 2001

Maisha yake

Jorge Bergoglio alizaliwa Buenos Aires, ni mmoja kati ya watoto watano watano wa  Baba wa kiItaliano aliyekuwa akifanya kazi katika Shirika la Reli nchini humo na mkewe. Baada ya kumaliza masomo yake ya Seminari huko Villa Devoto alijiunga na jumuiya ya Yesu Kristo mwezi Machi mwaka 11.03.1958 Bergoglio alijipatia shahada ya juu ya Filosofia katika chuo cha  Máximo San José huko San Miguel, na baadaye alifundisha Fasihi na saikolojia katika chuo cha Colegio de la Inmaculada huko Santa Fe, na chuo cha Colegio del Salvador huko Buenos Aires. alipata daraja takatifu la upadre  Desemba 13, 1969, aliopewa na Askofu Ramón José Castellano. alisomea masomo ya filosofia na Teolojia huko San Miguel.Bergoglio aliendelea huvyo na kuwa Professor wa Teolojia 

Papa Fransisco wa I akiwasalimia waamini wa Kanisa Katoliki na kutoa Baraka zake za kwanza kama Baba Mtakatifu huko Vatican
Kutokana na uongozi wake mzuri Jumuiya ya Kristo ilimteua Bergoglio kiongozi toka mwaka 1973 hadi 1979, mwaka 1980 alihamishwa na kuwa Rector katika Seminary ya San Miguel ambako alisomea pia . alihudumu katika Seminari hiyo hadi mwaka 1986

Bergoglio alipata daraja la Askofu mkuu tarehe 28.02.1998 huko Argentina, Papa John Paul wa II alimwita Vatican Askofu huyo mpya tarehe 21.02.2001 na kumpa heshima kuwa Kardinali wa Argentina.


 Kabla ya Kuteuliwa kuwa Baba Mtakatifu, Kardinali George Mario Bergoglio alishika nafasi mbalimbali za uongozi wa kanisa huko Roma na katika nchi yake pia, hivyo uongozi wake ulikubalika kwanzia nchini kwake na hata katika uongozi wa kaniza zima huko Vatican.











Breaking News: The New Pope Elected in Vatican



White Smoke through above the Sistine Chapel
White smoke appeared from the chimney above the Sistine Chapel, and bells from St. Peter's Basilica have pealed, meaning the 115 Roman Catholic cardinals gathered at the Vatican from all over the world have chosen a new pope. The church's 266th pontiff will replace Benedict XVI, whose surprise resignation last month prompted the cardinals to initiate a conclave, a Latin phrase meaning "with a key," to pick a new leader for the world's almost 2 billion Catholics.

Some of the Pastoric wears for the pope
Although it's not immediately clear who received the necessary two-thirds vote, several candidates were mentioned as front runners, including what could be the first African pope or the first pope from the U.S. or Canada. The new church leader takes over an organization many say is in crisis, from damaging allegations of internal squabbling to the cover-up and abetting of sexual abuse, though the latter issue came to light before Benedict's papacy. Some sources say the Catholic Church in the U.S. has paid out as much as $3 billion to settle sexual abuse claims, though others estimate a billion less. At least eight U.S. Catholic dioceses declared bankruptcy protection. Benedict said in a 1998 U.S. visit that he was ashamed of the sex abuse scandal, and assured that the church would not allow pedophiles to become priests.

The Pope Emeritus also faced criticism for his role in overseeing the church's reaction to the sexual abuse crisis, as well as revelations from the "Vatileaks" incident. The pope's butler was implicated in the leaking of documents that included what Italian media first characterized as evidence of blackmail and disarray among church leaders regarding how to address growing concerns about money laundering.

Shoes for the Pope
 Though Benedict basically dismissed those allegations as exaggerated, he remarked that the leaks and results of the ensuing investigation he commissioned had saddened him. Church outsiders have speculated that the results of Benedict's investigation may have led to his decision to resign from the papacy, a move unprecedented in six centuries.

The new pope will also face pressure to modernize the church on issues from reforming the clergy to allowing contraception. It's unclear if the cardinals will pick a pope who will change the church or a conservative leader who will remain dedicated to its current principals.

Thursday, March 7, 2013

WANAFUNZI 1,000 WASOMEA CHINI MPANDA


ZAIDI ya wanafunzi 1,000 wa Shule ya Msingi Mbugani, iliyopo Kata ya Kakese katika Halmashauri ya mji wa Mpanda wanasomea chini kutokana na ukosefu wa madawati unaoikabili shule hiyo.

Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Anthony Mbawa, alitoa taarifa hiyo jana kwa waandishi wa habari waliotembelea shule hiyo kwa lengo la kuangalia changamoto zinazoikabili shule hiyo.

Alisema shule hiyo ina wanafunzi 1,333 kati yao, 162 ndio wanaosoma wakiwa wamekaa kwenye madawati ambao wanasoma darasa la saba na la sita.

Alisema shule hiyo iliyoanzishwa mwaka 2002, ina madawati 54 kwa shule nzima.
Alieleza changamoto nyingine zinazoikabili shule hiyo kuwa ni mrundikano wa wanafunzi katika madarasa kutokana na uchache wa majengo ya madarasa.

Alitoa mfano kwa wanafunzi wanaosoma darasa la kwanza kwa kueleza kuwa lina wanafunzi 218 wanaosoma kwa wakati mmoja, hali ambayo inasababisha mwalimu kupata shida ya kutoa maelekezo kwa kila mwanafunzi.

Naye mwanafunzi wa darasa la nne, Jafe Thomas, alisema kitendo cha wao kusoma wakiwa wamekaa chini kunafanya washindwe kuandika vizuri.

Pia alisema sare zao zimekuwa zikichafuka kutokana na uchafu wa vumbi unaozagaa chini ya sakafu kwenye madarasa.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji wa Mpanda, Enock Gwambasa, alisema katika kukabiliana na tatizo hilo, Benki ya NMB Tawi la Mpanda imetoa ahadi ya kutengeneza madawati 100 yenye thamani ya sh milioni 15 kwa ajili ya shule hiyo.

Tanzania daima 
 

Monday, March 4, 2013

Mauaji siku ya kupiga kura Kenya


Mmoja wa wale waliojeruhiwa
 Taarifa ambazo bado hazijathibitishwa zinasema kuwa watu 10, wakiwemo maafisa wa polisi wawili, wameuawa mjini Mombasa, Pwani ya Kenya. Tukio hilo lilitokea alfajiri, kuamkia leo wakenya wanapopiga kura.
 
Hata hivyo polisi walithibitisha vifo vya maafisa wao wawili vilivyotokea wakati polisi walipowapiga risasi washambulizi waliokuwa wamejihami kwa mapanga. Lilikuwa shambulizi la kulipiza kisasi.
 
Washambulizi hao wanashukiwa kuwa wafuasi wa kundi la Pwani la Mombasa Republican Army (MRC) ambao wamekuwa wakipigania uhuru wa jimbo la Pwani.
 
Mwandishi wa BBC, Karen Allen, anasema polisi waliweza kuthibitisha vifo vya wanne katika eneo la Changamwe, naye Hassan Majid aliona mtu mmoja kauawa eneo la Mishomoroni. Mwtu mwingine Moja ya miili hiyo ilikuwa imekatwakatwa.
 
Zaidi ya watu 1,000 waliuawa miaka mitano iliyopita katika ghasia zilizotokea baada ya uchaguzi wa mwaka 2007.

MBOWE “AICHANA” SERIKALI MJINI MPANDA


  •   Asema kuhutubia mkutano bila kuitaja CCM au Viongozi wake  ni sawa na Kuhubiri injili bila kumtaja Shetani.
  • Tatizo la Udini liliasisiwa na CCM
  • Alia na janga la Elimu, asema ni bomu tusiloweza kulicontrol
  • Asisitiza serikali bila presha haiendi, mawaziri wa Elimu sharti wawajibike kwa matokeo mabaya ya kidato cha nne
  •  Asuluhisha Mgogoro uliokuwa ukifukuta ndani ya Chama

Freeman Mbowe na Said Arfi wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara  
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Freeman Aikael Mbowe jana amefanya mkutano wa hadhara katika viwanja vya Kashaulili mjini Mpanda ambapo mamia ya wakazi walihudhuria.

Akihutubia mkutano huo Mbowe alizungumzia masuala kadhaa ya kitaifa na kichama likiwemo suala la Askari polisi wa Tanzania, akisifu kazi yao katika Wilaya ya Mpanda kuwa wanafanya kazi kwa maadili na kuwataka Polisi sehemu nyingine Tanzania kuiga mfano wa Polisi Mpanda, akiwapongeza polisi hao amewaahidi kuwa CHADEMA ikishika Dola mwaka 2015 itakuwa pamoja nao.

Mbowe akizindua Harambee ya Ujenzi wa Ofisi ya Chama Mkoa
Katika mkutano huo ambao ulihudhuriwa pia na Viongozi wengine wa CHADEMA Mkoa na wilaya aliwataka wananchi kuipa nafasi CHADEMA kushika Dola mwaka 2015 na wakipime kwa utendaji kazi wake, iwapo wakishindwa basi “wakipige chini” na kuchagua chama kingine, “Biashara ya kufunga ndoa na chama cha siasa ni wendawazimu” alisema Mbowe. Akirejea maneno ya Mwalimu Nyerere  akisema CCM imepoteza mwelekeo, inanuka Rushwa.

Mbowe pia aliwataka vijana na jamii yote kuacha woga na kuchukua hatua ili kulinusuru taifa, kwani Serikali ya sasa bila Presha haiendi, akikumbushia suala la katiba Mpya Alisema Serikali isingekubali kuanza mchakato wa kuandika Katiba mpya kama isingetiwa Presha ndani na Nje ya Bunge.

Viongozi wa BAVICHA katika picha ya pamoja baada ya Mkutano
Akizungumzia tatizo na visa vya udini vinavyoendelea nchini, Mbowe amesema hayo ni matunda ya siasa za kibaguzi zilizoasisiwa na Chama Cha Mapinduzi, akifafanua kauli yake hiyo Mbowe amesema Mwaka 2000 CUF ilikuwa na nguvu na kuwa tishio kwa CCM, hivyo baada ya kuona Viongozi wa CUF wengi ni waislamu walitumia kigezo hicho kuwagawa wananchi kuwa wasichague CUF kwa kuwa ni chama cha Waislamu, amesema kitu hicho kilijenga ufa miongoni mwa jamii huku CCM wakifurahia ushindi, amesema pia kuwa baada ya kuona CHADEMA imekuja juu na kuwa tishio wanatumia mbinu ya Kuwagawa wananchi wakisema kuwa CHADEMA ni chama cha Kikristo, bila kujua wanaendeleza ufa waliokwisha utengeneza awali, hivyo matukio yanayotokea ni zao lililopandwa na CCM wenyewe hivyo hawana budi kulinywa.

Amesema CHADEMA hawachagui mtu kutokana na dini au kabila lake bali utendaji kazi na nia yake ya dhati ya kuihudumia jamii yake. Amesema katika ngazi ya CHADEMA Taifa yenye viongozi sita wanne kati yao ni Waislamu hivyo si sahihi kusema CHADEMA ni chama cha Kikristo, na pia si sahihi kusema CHADEMA ni chama cha Wachaga kwani katika uongozi wa Juu Mchagga ni Mbowe pekee, viongozi wengine wametoka katika makabila mbalimbali nchini.

Kabla ya Mkutano huo wa hadhara wa jana Mbowe alikuwa na kikao cha Ndani na Viongozi wa 
Mbowe akisalimiana na Mkazi wa Mpanda baada ya Mkutano
Chama Mkoa ambapo alisuluhisha migongano iliyokuwa imeanza kukitafuna chama, na katika mkutano wa hadhara Mbowe aliwasimamisha viongozi mbalimbali ambao kwa namna moja ama nyingine walihusika katika mgogoro huo nao walikiri hadharani kuacha tofauti zao na kuwa kitu kimoja na kufanya kazi kwa pamoja kwa maslahi ya Chama na Taifa kwa ujumla.

Katika Mkutano huo Mbowe aliongoza Harambee maalumu kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi ya Chama Mkoa ambao unapaswa kukamilika ndani ya mwaka mmoja. Katika harambee hiyo Mbowe aliahidi kuchangia Tsh. 5,000,000/- Wabunge wa CHADEMA waliahidi Mchango wa Tsh.1,500,000/= kila mmoja kwa ajili ya kununua kiwanja itakapojengwa ofisi. Katika harambee hiyo jumla ya fedha iliyochangwa ilikuwa Tsh. Milioni Kumi 10,000,000/= huku Fedha Taslimu zikipatikana Tsh. 200,000/=

Picha Zote na Khalfan Zozi

Friday, March 1, 2013

CHADEMA KUUNGURUMA MPANDA

  • Viongozi wa Kitaifa Kuhutubia.
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kinatarajia kufanya Mkutano Mkubwa siku ya Jumamosi ya Tarehe 02/03/2013 katika viwanja vya Kashaulili mjini Mpanda.

Taarifa za kuaminika kutoka kwa Katibu wa BAVICHA wilaya ya Mpanda Bwana Khalfan Zozi, alizozituma katika Mtandao wa CHADEMA Mkoani Katavi zinasema kuwa katika Mkutano huo, mambo mbalimbali ya Kitaifa yatazungumzwa na Viongozi hao wa CHADEMA Taifa.

Uongozi wa CHADEMA Mpanda Umewahamasisha wakazi wote wa Mpanda Mjini na Viunga vyake bila kujali itikadi za kisiasa kujitokeza katika viwanja vya Kashaulili ili waweze kusikia viongozi wa kitaifa wanasemaje na kufahamu msimamo wa CHADEMA kuhusu masuala mbalimbali yanayoendelea katika taifa kwa sasa.

Viongozi wanaotarajiwa kuhutubia Mkutano huo ni Freeman Aikael Mbowe (Mwenyekiti Taifa), Said Amour Arfi (Makamu Mwenyekiti Taifa) na Godbless Lema (Mbunge wa Arusha Mjini)

Akitoa ufafanuzi kuhusu Mkutano huo wa Jumamosi 02/03/2013 Bwana Zozi amesema mkutano huo pamoja na mambo mengine utahusu maandalizi ya awali uzinduzi wa kanda maalumu ya kichama (Kanda za Ziwa Tanganyika) ambayo itahusisha mikoa ya Katavi, Rukwa na Kigoma, pia amesema kuwa mkutano unalenga kujenga chama zaidi katika kuelekea Uchaguzi mkuu ujao.

CHADEMA kimekuwa ni chama kinachokua na kuungwa mkono na raia wengi kutokana na kufanya mikutano na kuwafikia wananchi wengi zaidi wakijipambanua kuhusu masuala mbalimbali ya kitaifa kupitia harakati mbalimbali kama Operation Sangara, na Movement For Change (M4C) ambazo zimesaidia kuondoa dhana kuwa Vyama vya Upinzani ni vyama vya Msimu vinavyoibuka kipindi cha uchaguzi na kupotea uchaguzi ukiisha.

KATAVI UP2DATE inawatakia mafanikio CHADEMA katika mkutano huo wa kesho Jumamosi tarehe 02.03.2013 uweze kufanyika na kumalizika salama.